Teknolojia
140 subscribers
3.87K photos
5.55K videos
94 files
13.7K links
Hii ni channel yangu mwenyewe ila kama ikikupendeza karibu isipokupendeza kwaheli 👋
Download Telegram
Tanzania Communications Regulatory Authority (Facebook)

“Pamoja kwa Mtandao Bora” #8/2/2022
Tanzania Communications Regulatory Authority (Facebook)

Washiriki wa Shindano la Tatu la masuala ya Usalama Mtandaoni 2021/22, wakishiriki fainali za Shindano hilo lililofanyika katika Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (CIVE-UDOM). Jumla ya washiriki 48 kutoka Taasisi mbalimbali za Elimu ya Juu wameshiriki Shindano hilo lililoandaliwa kwa lengo la kukuza uwezo kwa vijana katika kuimarisha na kukabili vihatarishi vya usalama mtandaoni.

Shindano hilo limeratibiwa na Kituo cha Kukabiliana na Majanga ya Kimtandao ( TZ-CERT) chini ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na kampuni ya Silensec. @tz_cert
TeknoKona (Facebook)

Februari 9 Samsung itazindua bidhaa hizi.
Tanzania Communications Regulatory Authority (Facebook)

Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) yamefanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam; jumla ya wanafunzi 354 kutoka Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo Vikuu wameshiriki.

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri Bakari, amewakilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Leseni Bw. John Daffa ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA Bi. Connie Francis, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Bw. Modestus Ndunguru pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Bw. Thadayo Ringo. Katika hafla hiyo, TCRA imekabidhi vyeti pamoja na zawadi kwa wanafunzi 4 walioibuka kidedea kwenye shindano la Tatu la masuala ya usalama mtandaoni “Cyberstar” lililofanyika katika ndak...

View original post
TeknoKona (Facebook)

WhatsApp toleo la kutumika kupitia kivinjari/kompyuta linaendelea kufanana kwa karibu na lile la kwenye simu janja.
Tanzania Communications Regulatory Authority (Facebook)

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeadhimisha Siku ya Usalama Mtandaoni kwa kutoa elimu kuhusu Usalama Mtandaoni kwa Wanafunzi na Wakufunzi wa Chuo cha Amali Daya kilichopo kisiwani Pemba. Zoezi hilo limeongozwa na Meneja wa Ofisi ya TCRA Zanzibar Bi. Esuvatie Aisa Masinga.

Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni Mwaka 2022 ni “Pamoja kwa Mtandao Bora”
TeknoKona (Facebook)

Hatari ya kufungwa kwa Facebook na Instagram huko Ulaya. Je, unafahamu sababu?
TeknoKona (Facebook)

Teknolojia inayoweza kutusaidia kufanya kilimo cha kisasa.
TeknoKona (Facebook)

Chukua tahadhari dhidi ya wadukuzi kwa kulinda usalama wa Taarifa zako binafsi. Tembelea tovuti yetu kwa ushauri zaidi https://zcu.io/2FLr
TeknoKona (Facebook)

Umechukua tahadhari gani dhidi ya wadukuzi kati ya zifuatazo?
1. Kutumia nywila imara
2. Kuzima kompyuta au simu yako unapotoka kwa muda au unapompa mtu akushikie
3. Kutofungua baruapepe ambayo...